Machapisho

Loka 7 matatizo

Picha

JINA LAKO LITUKUZWE #MATHAYO 6:9

Picha
JINA LAKO LITUKUZWE #MATHAYO 6:9 MPENDWA WANGU NIMEKUKUMBUSHA SEHEMU YA KILE TULICHOANDIKA KATIKA KITABU CHAKO CHA ‘KUWA NA UJUZI KATIKA MAOMBI’ UKURASA WA 14. HEBU JIFUNZE KITU KATIKA SEHEMU HII. -------------------------------- Mwana wa Mungu, Jina la kiumbe chochote kile duniani huwa lina akisi tabia ya kiumbe hicho. Nadhani wajua hata wewe unapenda uitwe kwa jina lako maana ndani ya jina lako limekubeba wewe mwenyewe. Majina huwa yanabeba tabia zetu. Majina huwa yana akisi tabia zetu. Ndiyo  maana wazazi wanashauriwa sana kuwa makini wanapowapa majina watoto wao. Ni lazima yaakisi maana halisi ya kile wanachotaka kukimaanisha. Sio vizuri kumpa mtoto jina ili mradi ni jina kwa sababu jina hilo hubeba tabia ya huyo mtoto. Wajua tena mara nyingi tu watu wengi unawaona mtaani tabia zao zinalingana kabisa na majina yao. Kwa nini? Kwa sababu nyakati zingine majina hayo hubeba roho zikisimamia tabia za majina hayo. Usimpe mtoto tu kwa sababu ni jina. Ndivyo ilivyo mwana wa Mungu kati

TUBUNI KWA MAANA UFALME WA MBINGUNI UMEKARIBIA.

Picha
TUBUNI KWA MAANA UFALME WA MBINGUNI UMEKARIBIA. Basi Yesu aliposikia ya kwamba Yohana amefungwa, alikwenda zake mpaka Galilaya;  akatoka Nazareti, akaja akakaa Kapernaumu, mji ulioko pwani, mipakani mwa Zabuloni na Naftali;  ili litimie neno lililonenwa na nabii Isaya, akisema,  Nchi ya Zabuloni na nchi ya Naftali, Njia ya bahari, ng'ambo ya Yordani, Galilaya ya mataifa,  Watu wale waliokaa katika giza Wameona mwanga mkuu, Nao waliokaa katika nchi na uvuli wa mauti Mwanga umewazukia. TOKEA WAKATI HUO YESU ALIANZA KUHUBIRI, NA KUSEMA, TUBUNI; KWA MAANA UFALME WA MBINGUNI UMEKARIBIA. #MATHAYO 4:12-17 Nakusalimu katika jina la Yesu Kristo mwana wa Mungu. Kwanza nikutakie ibada njema mpendwa wangu ambaye leo ni siku yako ya ibada. Kila siku ya jumapili huwa siachi kuzungumza jambo kwa ajili ya kanisa kuboresha ibada zetu.  Yamkini Neno hili katika #Mathayo 4:17 likawa si neno lenye kuhubiriwa kwa sauti kubwa na yenye nguvu katika baadhi ya madhehebu mengi lakini acha niseme jambo l

AMANI YA BWANA IWE NANYI.

Picha
KWA NEEMA YA MUNGU, leo ni siku ya Kukusanyika kwa ajili ya Ibada takatifu kabisa. Jiandae vyema na pia uwakumbushe watu wengine. MUNGU AKUBARIKI SANA. KATIKA JINA LA YESU KRISTO. *AMINA*